Image result for tigo banner

Sepp Blatter alazwa hospitali baada ya kupata mshituko

Rais wa shirikisho la Soka la kimataifa, Sepp Blatter aliyesimamishwa kwa siku 90 kujishughulisha na masuala ya soka kwa kashfa za rushwa, amelazwa hospitali kutokana na kupatwa mshtuko wa neva.
FIFA President Sepp Blatter speaks during a press conference on October 4, 2013 at the FIFA headquarters in Zurich. FIFA said they could not get involved in labour issues in any country, amid calls for action after claims that dozens of migrant workers had died on construction projects linked to the 2022 World Cup in Qatar. Blatter, however said that the federation could not turn a blind eye to the reports, which also alleged that thousands of other workers endured conditions akin to "modern-day slavery" in Qatar. AFP PHOTO / FABRICE COFFRINIFABRICE COFFRINI/AFP/Getty Images
Blatter amelazwa hospitali kwa ajili ya uchunguzi wa afya lakini sasa imeelezwa ataendelea kubaki huko. Awali ilidaiwa alikuwa na matatizo ya msongo wa mawazo hivyo ikabidi apate huduma ya matabibu, sasa imebainika ana tatizo la mshtuko wa neva.
Awali, mwanasheria wake, Richard Cullen alieleza juu ya uangalizi huo wa madaktari kutarajiwa, lakini akasema alitarajia arejee nyumbani mapema kabla hali kubadilika na kutolewa maelezo tofauti.
Hata hivyo, watu wake wa karibu wameeleza hali yake si mbaya na anatarajiwa kurejea katika hali ya kawaida japokuwa atabaki hospitalini hadi mapema wiki ijayo.
Msaidizi wake, Walter Gagg, amesema kwamba bosi huyo anatarajiwa kuwa mwenyeji wa hafla ya kukabidhi tuzo ya mwanasoka bora hapo Januari 11 mwakani.

No comments

Powered by Blogger.