Diamond aitambulisha rasmi lebo ya WCB pamoja na kumsainisha Rich Mavoko
Msanii
wa Muziki wa Kizazi kipya, Diamond Platnumz akisaini mkataba wa kufanya
kazi na msanii Rich Mavoko huku Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey
Mngereza akishuhudia tukio hilo. Nyuma ni uongozi wa WCB na msanii
Diamond.
Msanii
wa Muziki wa Kizazi kipya, Diamond Platnumz akibadilishana mkataba na
Rich Mavoko mara baada ya kusaini huku Katibu Mtendaji wa BASATA,
Godfrey Mngereza akishuhudia tukio hilo.
MSANII
wa Muziki wa Kizazi kipya, Diamond Platnumz amezindua rasmi Lebo ya
muziki ‘WCB Record Label’ na kuwatangaza wasanii wanaosimamiwa na lebo
hiyo huku msanii Rich Mavoko akisaini mkataba wa kufanya kazi na Lebo
hiyo katika Hoteli ya Regency jijini Dar es Salaam.
WCB
inakuwa ni lebo ya kwanza nchini Tanzania kuanzishwa na kusimamiwa na
mwanamuziki, ikilinganishwa na lebo kadhaa ambazo zilikuwa zikisimamiwa
na wadau waliokuwa katika tasnia ya sanaa na burudani.
Mkurugenzi
Mtendaji Mkuu WCB, Diamond Platinumz alisema lengo la kuanzishwa lebo
hiyo ni kusaidia vijana wenye vipaji na kuifanya sanaa ya muziki
izalishe pato la taifa.
Msanii
Diamond ameomba serikali kuwaunga mkono ili waweze kusonga mbele maana
kwa sasa amekuwa na watu kadhaa ambao wamekuwa wakimtegemea katika
kufanya sanaa ya muziki.
Post a Comment