Image result for tigo banner

Picha: Huyu ndiye aliyechukua nafasi ya Nay wa Mitego kwa Shamsa Ford

Kikohozi cha mapenzi kinaendelea kumkaba malkia wa filamu Shamsa Ford. Baada ya kupigana chini na rapper Nay wa Mitego na kuapa kutomwanika tena mpenzi wake mpya katika mitandao ya kijamii, Jumamosi hii hali imemshinda na kuanza kushare picha mbalimbali akiwa na mtu wake wa karibu.
mmk
Muigizaji huyo mahiri wa filamu ambaye ni mama wa mtoto mmoja, miezi michache iliyopita baada ya kuachana na Nay wa Mitego, aliaambia Bongo5 kuwa hatarudia tena kushare picha za mpenzi wake katika mitandao ya kijamii.
Mrembo huyo Jumamosi hii ameshare picha mbalimbali katika mtandao wa kijamii akiwa na mtu wake wa karibu na kuandika ujumbe huu:

Kuna muda unaweza ukafanya kitu mtu akakuona mshamba au limbukeni. Ila ukweli ni kwamba hakuna mtu anaweza jua hisia za mwenzie anavyojisikia kwa wakati ule zaidi ya yeye mwenyewe. .TUHESHIMU HISIA ZA WENZETU. …I love you a man of my dream…NICE Saturday
4K0A7304
mm

No comments

Powered by Blogger.