Wanafunzi ambao 'hawakufuzu' kufukuzwa vyuoni TZ
Maelfu ya wanafunzi
wa vyuo na vyuo kikuu nchini Tanzania wako hatarini kufukuzwa katika
vyuo hivyo baada ya mamlaka kugundua kashfa kubwa inayohusisha usajili
wa wanafunzi ambao hawakufuzu.
Magazeti ya the Guradian na Citizen nchini humo yanasema kuwa serikali imewafukuza wanafunzi 489 ambao walikuwa wamesajiliwa katika chuo kikuu cha St Joseph na kupewa mikopo ya serikali licha ya kuwa hawakufuzu kusomea ualimu.
Serikali imefunga chuo hicho kikuu kazkazini na kusini mwa Tanzania.
Post a Comment