Image result for tigo banner

Nuh Mziwanda: Haikuwa rahisi kumshirikisha Alikiba, ni heshima kubwa kwangu

Nuh Mziwanda amesema kumpata Alikiba na kumshirikisha kwenye wimbo wake halikuwa jambo rahisi na kwamba kwake hiyo ni heshima kubwa.
Mziwanda 2452524_n

Anadai kawa wimbo huo ulichukua muda kuurekodi kutokana na ratiba ngumu ya Alikiba.

“Nimegundua kwamba nina uwezo, yeye ana uwezo mkubwa ambao kumbe hata msanii kama Alikiba anaanza kutoka mimi namsikia bado mdogo, ameweza kufanya collabo na mimi kiroho safi sababu ni msanii mgumu sana kufanya naye collabo,” Nuh amesema

“Kwahiyo imenipa moyo na kuona kwamba kumbe mimi ni mwanamuziki sio mbabaishaji. Kuna credit kubwa sana ambazo nimezipata na ushauri mkubwa pia anaokuwa ananipa,” ameongeza.
Nuh alimshirikisha Alikiba kwenye wimbo wake Jike Shupa.

No comments

Powered by Blogger.