PSG na Real Madrid wako kwenye mazungumzo ya kumsajili Jese Japo kuwa ye Anaitaka Liverpool
PSG na Real Madrid wako kwenye mazungumzo ya
kumsajili Jese Japo kuwa ye Anaitaka Liverpool
Mshambuliaji wa Real Madrid Jese Rodriguez anategemea kuhama
mabingwa wa ligi ya Ulaya Real Madrid. Jese amekaa benchi kwa michezo mingi
iliyo chezwa na mabingwa hao. Japo kuwa alikuwa anasumbuliwa na majeraha ila
hakuweza kupata mda mwingi wa kucheza alipo pona.
Jese anamua kutoka Real Madrid ili kipaji chake cha kucheza
kisiweze kupotea. Vyombo vya habari mchana wa leo vimeripoti kuwa Klabu ya
Ufaransa Paris Saint German (PSG) wako mbioni kunasa saini ya mshambuliaji huyo
japo kuwa mchezaji huyo amesema anataka kujiunga na majogoo Liverpool Fc. Jese
anahitajika ili aweze kutengeneza safu ya ushambuliaji akiwa na Cavan baada ya
kuondoka kwa Ibrahmovic.
Dalili za wazi zinaonyesha kuwa Jese atajiunga na PSG kwa
kuwa kocha wa PSG Unai Emery anampenda mshambuliaji huyo maana alitaka kumsajili
kipindi alipo kuwa kocha wa Sevilla.
Post a Comment