TTCL yazindua Nembo (Logo) mpya na Huduma ya 4G LTE
Katika uzinduzi wa nembo mpya ya TTCL, Waziri Mbarawa amesema “TTCL
lazima mubadilike ili muweze kuendana na kasi ya mabadiliko ya sayansi
na teknolojia na hivyo kumudu ushindani uliopo sasa katika sekta ya
mawasiliano.”
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza
na wafanyakazi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), na wadau wa Sekta ya
Mawasiliano (hawapo pichani), wakati uzinduzi wa nembo mpya ya kampuni
hiyo na huduma ya 4G LTE jijini Dar es Salaam.
Mjumbe
wa Bodi ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bi. Edwina Lupembe
akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa
Makame Mbarawa, katika hafla ya uzinduzi wa nembo mpya ya kampuni hiyo
na huduma ya 4G LTE
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dkt. Kamugisha
Kazaura akielezea mafanikio ya TTCL kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani), katika hafla ya
uzinduzi wa nembo mpya ya kampuni hiyo na huduma ya 4G LTE jijini Dar es
Salaam.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizindua
nembo mpya ya Kampuni ya Simu ya Tanzania (TTCL), jijini Dar es Salam.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akijadiliana
jambo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dkt.
Kamugisha Kazaura, wakati wa halfla ya uzinduzi wa nembo mpya ya kampuni
hiyo na huduma ya 4G LTE jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), wakifatilia sherehe
za uzinduzi wa nembo mpya ya kampuni hiyo na huduma ya 4G LTE jijini Dar
es Salaam.
Post a Comment